Warumi
Warumi

Search Course

Type at least 3 characters to search

Search through all lessons and sections in this course

Searching...

No results found

No matches for ""

Try different keywords or check your spelling

results found

Lesson 6: Ushindi dhidi ya Dhambi

26 min read

by Stephen Gibson


Dhambi

Warumi 6 inahusu ukombozi kutokana na nguvu ya dhambi. Ili tuweze kuelewa toba na ushindi, ni lazima tuelewe dhambi ni nini.

► Dhambi ni nini?

Kwa kawaida Biblia huzungumzia kuhusu matendo ya dhambi kama yanayofanywa kwa hiari (1 Yohane 3:4-9, Yakobo 4:17). Wakati mtu anapofanya kwa kukusudia na kwa kujua akachagua kutokumtii Mungu, hiyo ni dhambi ya kujitakia au hiari.

Kuna utendaji wa bila kufahamu au ukiukaji wa bahati mbaya wa sheria ya Mungu hauvunji sheria au uhusiano na Mungu kama dhambi ya kukusudia inavyofanya. Tunapokuwa tunatembea kwenye nuru (tukiishi kulingana na ukweli tunaoujua), tunatakaswa na aina zote za dhambi (1 Yohane 1:7) na haihitajiki kuwa kwenye mashaka kwamba ukiukaji unaofanyika kwa bahati mbaya utatutenganisha na Mungu.

Kimsingi kifungu hiki kinazungumzia kuhusu dhambi za kujitakia au za hiari, ambazo huharibu Imani na kuleta madhara katika uhusiano wa mtu na.