Warumi
Warumi

Search Course

Type at least 3 characters to search

Search through all lessons and sections in this course

Searching...

No results found

No matches for ""

Try different keywords or check your spelling

results found

Lesson 10: Ujumbe wa Haraka

17 min read

by Stephen Gibson


Kifungu cha kujifunza – Warumi Sehemu 5, kifungu cha 2-3

Warumi 10 ni kilele cha kitabu cha Warumi. Mtume tayari alishaeleza kwamba wokovu ni kwa neema kwa njia ya imani na kwamba kila mtu katika ulimwengu huu anauhitaji. Kwa kuwa imani ni ya lazima, ujumbe wa injili ni muhimu: Watu wanahitaji kusikia ujumbe ili kwamba waweze kuuamini. Sura hii ni ya muhimu katika kusudi la kitabu kwa sababu kitabu chote kinatoa msingi wa kazi ya umishenari.

Warumi 11 inahusika na mahusiano kati ya Waisraeli na Kanisa. Wayahudi wengi waliikataa injili. Paulo alielezea kwamba mpango wa Mungu ulikuwa ni dunia yote pamoja na Wayahudi waweze kuokolewa. Waisraeli kwa ujumla wao kuna siku moja watakayomkubali Kristo.