Mafundisho Na Mazoezi Ya Kanisa
Mafundisho Na Mazoezi Ya Kanisa

Search Course

Type at least 3 characters to search

Search through all lessons and sections in this course

Searching...

No results found

No matches for ""

Try different keywords or check your spelling

results found

Lesson 7: Kanisa katika Dunia

11 min read

by Stephen Gibson


Kanisa katika Jamii

► Je, ni kwa jinsi gani kanisa lihusike ndani ya jamii?

Yeremia aliandika kwa Wayahudi akiwa utumwani akiwaambia kuhusu uhusiano wao utakavyokuwa kati yao na jamii ya kipagani waliokuwemo. Wayahudi hawa walikuwepo utumwani pasipo matakwa yao; dini ya jamii iliyokuwepo ilikuwa ya kipagani; serikali iliyokuwepo ilikuwa ya ugandamizaji iliyoharibu taifa lao; na, walikuwa wakingojea siku ambayo wangeondoka. Labda walifikiri hawangejihusisha na matatizo yeyote ya jamii ile.

Sikiliza ujumbe ambao Mungu alimpa Nabii kwa ajili ya watu hawa:

Kautakieni amani (shalom) mji ule, ambao nimewafanya mchukuliwe mateka, mkauombee kwa Bwana; kwa maana katika amani yake mji huo ninyi mtapata amani (Yeremia 29:7).

[1]Shalom, neno hili kwa kawaida likiwa linatafsiriwa kwamba ni amani, halirejelei tu amani peke yake, bali pia baraka zinazoambatana na amani. Linarejea baraka zinazotoka kwa Mungu. Hawa watu waliokuwa wakimwabudu Mungu katika nchi ya wapagani wanaenda kupata baraka wanapokuwa wanajaribu kuzileta baraka hizo kwa watu wa jamii ya makafiri!

Matatizo ya dunia yanatokana na chanzo chake cha ndani cha tatizo la dhambi. Watu binafsi na mataifa yenye nguvu yaliyojipanga vizuri hawaheshimu Neno la Mungu. Kanisa ndilo pekee lenye sifa ya kuweza kuzungumzia matatizo ya dunia kwa sababu kanisa lina uwezo wa Kufafanua Neno la Mungu na kudhihirisha hekima ya Mungu. Kanisa halipaswi tu kuzungumzia na kuwa kinyume cha dhambi zilizopo katika jamii, bali pia kufafanua na kudhihirisha ni kwa jinsi gani jamii inapaswa ifananie.


[1]

“Kanisa la Kikristo ni jumuiya ambamo Roho Mtakatifu hupitia kwa ajili ya kuongoza ukombozi na ugawaji wa karama, njia ambayo Mungu huitumia kufanyia kazi yake ya upatanisho katika Kristo aliyeko kwa wanadamu. Kanisa limeitwa kutoka katika dunia ili kusherehekea ujio binafsi wa Mungu, na limetakiwa lirejee duniani kwa ajili ya kutangaza ufalme wa Mungu ulio kiini cha ujio binafsi wa Mungu na tegemeo la kurejea tena alikotoka.”

- Thomas Oden,
Life in the Spirit