Uinjilisti Wa Kibiblia Na Uanafunzi
Uinjilisti Wa Kibiblia Na Uanafunzi

Search Course

Type at least 3 characters to search

Search through all lessons and sections in this course

Searching...

No results found

No matches for ""

Try different keywords or check your spelling

results found

Lesson 12: Milango iliyofunguka

11 min read

by Stephen Gibson


Utangulizi

► Je, kuna ulazima wowote wa kuomba kwa ajili ya wenye dhambi? Je, ni mahali gani kwenye Bibilia tunapoagizwa kwamba tuombe kwa ajili ya wenye dhambi?

Siyo rahisi kupata aya kwenye Biblia inayosema moja kwa moja kwamba tunapaswa tuombe kwa ajili ya mabadiliko ya wenye dhambi. Kitu tunachoweza kukipata ni aya nyingi zinazotueleza kwamba tunapaswa kuomba kwa ajili ya ufanisi wa usambazaji wa injili (2 Wathesalonike 3:1, Waefeso 6:19, Wakolosai 4:4, Matendo 4:29).

Hatujui kwamba tunapaswa tuombe kwa ajili mabadiliko ya wenye dhambi pamoja na kuomba kwa ajili ya ufanisi wa usambazaji wa injili. Tunaambiwa tuombe kwa kila mtu, ikiwa ni pamoja na kuomba kwamba wenye dhambi wapate kubadilika (1 Timotheo 2:1). Tunaambiwa tujaribu kuleta watu kwenye toba, (2 Timotheo 2:25 ). na litakuwa jambo sahihi kuomba msaada wa Mungu kwenye kazi hiyo.